Usiku wa Jumamosi ya Tarehe 30.Augost 2014, majira ya saa 10 alfajiri
Mwanamuziki nyota wa Bongo Flaver Nasib Abdul aka Diamond Platnumz alijukuta katika
hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini Stuttgart,Ujerumani,baada
ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri onyesho
lake,washabiki hao waliokuwa wamelipa tiketi kwa Euro 25 kwa kiingilio
waliahidiwa kuwa onyesho lingeanza saa 4.00 usiku, lakini walijukuta
wakisubiri hadi majira ya saa10 usiku au alfajiri ndipo mwanamuziki
Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake raia wa Nigeria anajiita kama Britts Event.
Hapo
ndipo washabiki walipoona kuwa hawakutendewa haki walianza kurusha
chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki Diamond na promota wake,
Kilichowakera
zaidi washabiki ni pamoja na vyombo vibovu vilivyofungwa katika ukumbi
huo kitu ambacho kiliwafanya washabiki kuvunja hadi vyombo vya muziki
Ma-Djs walishambuliwa na wapo Hosptalini kwa sasa.
moja wa Djs hao alipoteza Lap top yake ,mwanadada DJ Flor alipatwa na mshtuko wa moyo na kukimbizwa hosptali, washabiki hao walimpa kipigo DJ Drazee naye yupo hoi hospatalini .
Polisi
nchini Ujerumani wanamesema tukio hili la aibu halijawahi kutokea,kwa
msanii kuchelewa kufika jukwaani kwa ujerumani ni kitu cha hatari kwani
washabiki wa ujerumani wanaheshimu sana muda wao.
mpaka sasa polisi wanamsaka mwandaaji wa onyesho hilo na wamesema kuwa
wanachunguza
thamani ya hasara hiliyosababishwa na ghasia hizo na pia itamfungulia
mashataka promota huyo raia wa Nigeria,ambaye pia anachunguzwa kwani
inasemekana anajihusisha na mtandao fulani wa biashara.
Magazeti ya Stuttgart; yameandika kwa kijerumani “Washabiki wana hasira nawewe DIAMOND” kwenye link hii hapa:
No comments:
Post a Comment