Pages

KAPIPI TV

Monday, September 1, 2014

POLISI UJERUMANI WAMUOKOA DIAMOND KUTOKA KWA WASHABIKI WENYE HASIRA

huu ndio ukumbi uliharibiwa na washabiki mjini stuttgart,ujerumani-1Stuttgart,Ujerumani,
Usiku wa Jumamosi ya Tarehe  30.Augost 2014, majira ya saa 10 alfajiri
Mwanamuziki nyota wa Bongo Flaver  Nasib Abdul aka Diamond Platnumz alijukuta katika hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini Stuttgart,Ujerumani,baada ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri onyesho lake,washabiki hao waliokuwa wamelipa tiketi kwa  Euro 25 kwa kiingilio waliahidiwa kuwa onyesho  lingeanza saa 4.00 usiku, lakini walijukuta wakisubiri hadi majira ya saa10 usiku au alfajiri ndipo mwanamuziki Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake raia wa Nigeria anajiita kama Britts Event.
 
Hapo ndipo washabiki walipoona kuwa hawakutendewa haki walianza kurusha chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki  Diamond na promota wake,
Kilichowakera zaidi washabiki ni pamoja na vyombo vibovu vilivyofungwa katika ukumbi huo kitu ambacho kiliwafanya washabiki kuvunja hadi vyombo vya muziki
Ma-Djs walishambuliwa na wapo Hosptalini kwa sasa.
 
moja wa Djs hao alipoteza Lap top yake ,mwanadada DJ  Flor alipatwa na mshtuko wa moyo na kukimbizwa hosptali, washabiki hao walimpa kipigo  DJ Drazee naye yupo hoi hospatalini .
 
Polisi nchini Ujerumani wanamesema tukio hili la aibu halijawahi kutokea,kwa msanii kuchelewa kufika jukwaani kwa ujerumani ni kitu cha hatari kwani washabiki wa ujerumani wanaheshimu sana muda wao.
 
mpaka sasa polisi wanamsaka mwandaaji wa onyesho hilo na wamesema kuwa
wanachunguza thamani ya hasara hiliyosababishwa na ghasia hizo na pia itamfungulia mashataka promota huyo raia wa Nigeria,ambaye pia anachunguzwa kwani inasemekana anajihusisha na mtandao fulani wa biashara.
 
Magazeti ya Stuttgart; yameandika kwa kijerumani  “Washabiki wana hasira nawewe DIAMOND”  kwenye link hii hapa:

No comments: