Jaji
Constancia Gabusa (wa sita kutoka kushoto) akizungumza na mtoto Abdalah
Suleman (kulia) aliyefika kisimani kuchota maji katika kijiji cha
Chanjagaa wilayani Same. Mradi wa kisima hicho unafadhiliwa na kampuni
ya uchimbaji wa madini aina ya bauxite ya Willy Enterprises Ltd
Timu
ya majaji na sekretarieti ikiangalia bidhaa za urembo zinazotengenezwa
na kikundi cha wakinamama wa kimasai cha Ebeneza mara walipotembelea
kikundi hicho huko Mirerani. Kikundi hicho kinafadhiliwa na kampuni ya
TanzaniteOne ikiwa ni pamoja na kutangaza bidhaa zake nchini Marekani.
Muuguzi
wa zahanati ya Mteke iliyopo wilayani Same Bi. Winfrida Momoya (kulia)
akizungumza na majaji Bw. Venance Bahati ( wa pili kutoka kushoto) na Bi
Constancia Gabusa (wa tatu kutoka kushoto) mara walipotembelea zahanati
hiyo inayofadhiliwa na kampuni ya uchimbaji wa madini aina ya bauxite
ya Willy Enterprises Ltd
Mkurugenzi wa mgodi wa madini ya vito wa TanzaniteOne Bw. Farai Manyemba akisisitiza jambo katika kikao hicho
Mkurugenzi
wa mgodi wa madini ya vito wa TanzaniteOne Bw. Farai Manyemba akielezea
mchango wa kampuni hiyo katika huduma za jamii mara timu ya majaji na
sekretarieti ilipofanya ziara kwenye mgodi huo
Jaji
Constancia Gabusa (kushoto) akioneshwa urembo na kupewa maelezo na mama
wa kimasai ambaye jina lake halikupatikana mara moja juu ya shughuli
zinazofanywa na kikundi cha wakinamama wa kimasai cha Ebeneza
kinachofadhiliwa na kampuni ya TanzaniteOne.
No comments:
Post a Comment