Pages

KAPIPI TV

Monday, September 1, 2014

JOPO LA MAJAJI TUZO YA RAIS YA HUDUMA ZA JAMII NA UWEZESHAJI LATUA KANDA YA KASKAZINI

Picha Na 2Jaji Constancia Gabusa (wa sita kutoka kushoto) akizungumza na mtoto Abdalah Suleman (kulia) aliyefika kisimani kuchota maji katika kijiji cha Chanjagaa wilayani Same. Mradi wa kisima hicho unafadhiliwa na kampuni ya uchimbaji wa madini aina ya bauxite ya Willy Enterprises Ltd
C360_2014-08-27-23-58-06-465Timu ya majaji na sekretarieti ikiangalia bidhaa za urembo zinazotengenezwa na kikundi cha wakinamama wa kimasai cha Ebeneza mara walipotembelea kikundi hicho huko Mirerani. Kikundi hicho kinafadhiliwa na kampuni ya TanzaniteOne ikiwa ni pamoja na kutangaza bidhaa zake nchini Marekani.
Picha Na 3Muuguzi wa zahanati ya Mteke iliyopo wilayani Same Bi. Winfrida Momoya (kulia) akizungumza na majaji Bw. Venance Bahati ( wa pili kutoka kushoto) na Bi Constancia Gabusa (wa tatu kutoka kushoto) mara walipotembelea zahanati hiyo inayofadhiliwa na kampuni ya uchimbaji wa madini aina ya bauxite ya Willy Enterprises Ltd
Picha Na 4Mkurugenzi wa mgodi wa madini ya vito wa TanzaniteOne Bw. Farai Manyemba akisisitiza jambo katika kikao hicho
Picha Na 5Mkurugenzi wa mgodi wa madini ya vito wa TanzaniteOne Bw. Farai Manyemba akielezea mchango wa kampuni hiyo katika huduma za jamii mara timu ya majaji na sekretarieti ilipofanya ziara kwenye mgodi huo
Picha Na 7Jaji Constancia Gabusa (kushoto) akioneshwa urembo na kupewa maelezo na mama wa kimasai ambaye jina lake halikupatikana mara moja juu ya shughuli zinazofanywa na kikundi cha wakinamama wa kimasai cha Ebeneza kinachofadhiliwa na kampuni ya TanzaniteOne.
Picha Na. 8Mkazi wa kijiji cha Kolila, King’ori Bw. Petro Losina akitoa maelezo kuhusu kisima cha maji kilichofadhiliwa na kampuni ya usagaji wa kokoto na utengenezaji wa matofali ya Arusha Aggregates Ltd. mbele ya majaji.

No comments: