Waziri
wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akipanda
mti wa pili aina ya mtiki ikiwa ni ishara ya kuthamini, kuhifadhi na
kutunza mazingira nchini wakati wabunge wa bunge hilo walipotembelea
Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) jana mjini Bagamoyo.Spika
wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) Dkt. Margaret Zziwa
akipanda mti aina ya mtiki ikiwa ni ishara ya kuthamini, kuhifadhi na
kutunza mazingira nchini wakati wabunge wa bunge hilo walipotembelea
Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) jana mjini Bagamoyo.
……………………………………………………
Na Eleuteri Mangi- MAELEZO
Spika
wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) Dkt. Margaret Zziwa
ameipa heshima Tanzania kwa kupanda mti aina ya mtiki ikiwa ni ishara ya
kuthamini, kuhifadhi na kutunza mazingira nchini.
Spika
Dkt. Zziwa alipanda mti huo wakati wa ziara yake pamoja na wabunge wa
EALA walipotembelea Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)
jana mjini Bagamoyo.
“Huu
ni utaratibu wetu na ni azimio tuliojiwekea kama EALA kupanda miti kila
tunapoenda kufanya mkutano katika nchi washirika ndani ya jumuiya yetu
ili kuwasisitiza wananchi umuhimu wa kutunza mazingira” alisema Dkt.
Zziwa.
Dkt.
Zziwa alisema kuwa imekuwa desturi ambayo pia ni utaratibu
waliojiwekea bunge hilo kupanda miti kila wanapokuwa na mkutano kila
mwaka katika nchi washirika ambapo mikutano hiyo hufanyika kwa mzunguko
ndani ya jumuiya.
Dkt.
Zziwa alieleza kuwa zoezi la kupanda miti hiyo lilikuwa lifanyike Dar
es Salaam lakini yeye na wabunge wa EALA waliamua lifanyike Bagamoyo
ambapo pamoja na kutembelea Taasisi ya TaSUBa wamepata kujionea hazina
ya historia Afrika Mashariki iliyopo katika mji mkongwe wa Bagamoyo.
Aidha,
Dkt. Zziwa amempa jukumu la Mbunge wa EALA kutoka Tanzania ShyRose
Bhanji kutembelea taasisi hiyo na kujionea hali ya miti waliyoipanda
wakati wa ziara yao inavyoendelea kumea na kutoa taarifa mara kwa mara
katika bunge hilo.
Kwa
upande wake Mbunge wa EALA kutoka Tanzania Makongoro Nyerere ametoa
wito kwa Watanzania wa kutunza mazingira kwa kupanda miti mingi
iwezekanavyo ili kutunza mazingira.
Makongoro amesema kuwa ni wajibu wa kila mwananchi ahamasike, kila mwananchi mmoja mmoja apande mti mmoja autunze hadi ukue.
Makongoro
alisisitiza kwa kusema, “Miti ina umuhimu mkubwa sana katika jamii
yetu, inasaidia kutunza uso wa ardhi yetu na rutuba kwa manufaa ya
kilimo bora katika nchi yetu’’.
“Miti
ni uchumi katika nchi, inatumika kujengea, kutengenezea samani za
maofisini na majumbani, viwandani kutengeneza vitu mbalimbali ikiwamo
viberiti na vyombo vya kusafiria vya baharini” alisema Makongoro.
Aidha,
Makongoro alisema kuwa kutokana na hatari ya mabadiliko hali ya tabia
nchi yanavyoendelea, ni wajibu wa kila Mtanzania kutunza mazingira na
kuzingatia usemi wa “Kata mti, Panda miti” ili kuboresha hali ya hewa
nchini na mazingira yawe rafiki kwa viumbe vyote vilivyopo kwenye maji
na nchi kavu wakiwemo wanyama, mimea, samaki na viumbe wengine wanaoishi
kwenye maji.
Katika
tukio la upandaji miti, ilipandwa jumla ya miti mitatu katika taasisi
ya TaSUBa ikiwa ni juhudi zinazofanywa na bunge la EALA katika kutunza
mazingira kwa vitendo.
Mti
wa pili ulipandwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dkt. Fenella Mukangara na wa tatu ulipandwa na Naibu Waziri wa Wizara ya
Ushirikiano ya Afrika Mashariki, Dkt. Abdala Juma Abdulla Saadalla.
No comments:
Post a Comment